JUSTICE_ PRISON WALIKALE
Mratibu wa shirika Bureau d’Etude et d’Appui au Développement de Walikale anatahadharisha wakuu viongozi kuusu hatari inayoletwa na wafungwa wa kijeshi wanao kuwa ndani ya gereza kuu la mtaa hio. Obedi Kamala anasema hivi kwa sababu ana hakika kwamba gereza hii haieneze tena masharti ya kulinda vizuri wafungwa. Anazungumziya hasa seli zisizo na milango tena. Kulingana naye, hali hii imedumu karibuni miezi sita tangu wafungwa wamoja wa kijeshi waliendesha fujo kali hadi kubomowa milango ya gereza kwaku dai malipo yao. Mtetezi huyu wa haki za binadamu anaeleza kwamba wengi kati ya wafungwa hawa wanabaki gerezani kwa utashi wao kwani hakuna kinachowazuia kutoroka. Hata hivyo, anatambua juhudi za viongozi kwa kulinda gereza hii lakini anadhani kuwa ni lazima kutenda mengi zaidi.
Ajouter un commentaire