PRISON CENTRALE DE WALIKALE
Wanajeshi makumi ine na mbili wanao fungwa katika gereza kuu la Walikale walidai Alhamisi iliyopita mishahara yao ya miezi kumi na mbili. Administreta wa mtaa ya Walikale ambaye anat hakikisha habari hii ana julisha kuwa wanajeshi hao wali vunja mlango wa gereza hilo na ku tiya vurugu kwa kurusha vitu kwenye jengo hilo. Kamishna mkuu KASONGO KABUNDA Ado Laurent anafichua kuwa ilibidi polisi iungane na jeshi ili utulivu urejeye humo. Hawa walitumiya risasi kwaku tuliza wafungwa hao. Hata hivyo, anahakikisha kuwa hakuna kisa cha kifo wala chakuumiya kilicho ripotiwa. Kiongozi huyu ana laani tukio hii na anaomba uongozi wa kijeshi wa jimbo la Kivu Kaskazini kutatua tatizo hili kwa haraka.
Audio
Ajouter un commentaire