SOCIAL
“Ajali za barabarani, magonjwa yenye kutokana na uchafu, ubandiya, unyanyasaji wa kiuchumi na kingono ni miongoni mwa hatari zinazo kumba watoto kadhaa wa mitaani ama maibobo wanao onekana kwa uwingi siku hizi katika barabara mbali mbali za mji wa Goma. » Tahadhari hii ni ya msimamizi wa Comité Urbain des enfants Mjini Goma. Richard MIVIRI anasema ya kuwa amegundua kuwepo kwa watoto wengi mjini Goma wa umri wa miaka chini ya kumi na mbili wanao zagaa zagaa waki omba omba barabarani, kwenye maduka na mikahawa. Anaongeza kuwa wengine wana pita nyumba kwa nyumba kwa kuomba misaada. Ana dhani kuwa hali hii inatokana na kuwepo kwa wahami wa vita kadhaa wasio pewa misaada ipasavyo katika kambi mbali mba za mji mkuu wa Kivu Kaskazini. Mtetezi huyu wa haki za watoto anatoa wito kwa serkali ya Kongo kutatua tatizo hili haraka iwezekanavyo.
Catégorie
Audio
Ajouter un commentaire